Thursday, March 9, 2023

FATUMAAAAAA, hebu muone Shaaban Dede live akiimba kibao hiki

 Ilikuwa ni siku ya pambano kati ya Sikinde na Msondo katika ukumbi wa Diamond Jubilee, nikiwa na camera yangu nikabahatika kurekodi kitu hiki kitamu sana...tufurahi wote. Usisahau kusubscribe na ku like ili niwe na nguvu za kuendeleza Tanzania Music Channel hii.


MIAKA KADHAA ILIYOPITA MSONDO NGOMA WALIKUWA JUKWAANI PALE LEADERS CLUB, ILIKUWA SIKU YA WACHAGA

 KATIKA MAKTABA YANGU NIMEKUTA VIDEO HII YA MSONDO NGOMA BABA YA MUZIKI TANZANIA. SIKU HII WALIKUWA JUKWAANI LEADERS CLUB KUSHEREHEKEA 'CHAGA DAY'.  HEBU TUFURAHI PAMOJA. LAKINI  USIKOSE KUSUBSCRIBE CHANNEL HII ITAKAYOKULETEA MAMBO MENGI YA MUZIKI WA ZAMANI, KAMA UNANENO ONGEA AU ULIZA




Wednesday, March 8, 2023

HATIMAE MSHINDI WA KWANZA NA WA PILI WA TOP TEN SHOW 1988

 HAWA hapa ndio waliokuwa washindi wa Top Ten Show 1988 Salna 5 Brothers toka Tanga na MK Group. Bahati mbaya bendi zote zilizofikia kumi bora mwaka ule (1988), International Safari Sound (Ndekule), Mwenge Jazz band, Varda Arts, Super Matimila, Tancut Almasi Orchestra, Vijana Jazz Band,  Maquis Original, Sambuluma Band, Salna Brothers na MK Sound. Ni Mwenge Jazz band na Varda Arts tu ambao wanafanya maonyesho mpaka leo. Vijana Jazz Band haieleweki kama bado iko au ndio nayo imekufa rasmi.

Hebu sikiliza kilichojiri.





KAMERA YANGU ILIREKODI DDC MLIMANI PARK WAKIPOROMOSHA KIBAO HIBA

 SIKU HII ILIKUWA UMETAYARISHWA MPAMBANO KATI YA MSONDO NA SIKINDE KATIKA UKUMBI WA DIAMOND JUBILEE.....KAMERA YANGU IKAREKODI WANA DDC MLIMANI PARK...HEBU FAID 'LIVE' HII UTADHANI IMEREKODIWA STUDIO. WALALE PEMA WOTE WALIOTANGULIWA MBELE YA HAKI



Tuesday, March 7, 2023

Saturday, March 4, 2023

MSHINDI WA SITA NA WATANO MASHINDANO YA BENDI MWAKA 1988


 HAKIKA kumekuwa na utata kuhusu mashindano ninayoyaongelea ni ya mwaka gani. Mashindano ya bendi ambayo yalifahamika kama Top Ten Show yalifanyika mara mbili.  Kwa mara ya jkwanza yalifanyika mwaka 1988 na mara ya pili yakafanyika kuanzia tarehe 29 Julai 1989 na kumalizika tarehe 25 Novemba mwaka 1989. 

Katika mashindano ya kwanza kila bendi ilipewa uhuuru wa kuchagua nyimbo moja  ambayo ishiriki katika mashindano hayo. Katika mashindano ya pili bendi zilipewa nafasi tatu, ya kwanza ni wimbo wowote ambao bendi ingechagua nafasi ya pili ilikuwa ni wimbo wenye'tuni' asili na wimbo wa tatu ulipea jina Afrika Nakulilia.

Mashindano ambayo mnayasikia hapa ni ya shindano la kwanza la 1988. Nategemea wote tunaenda sawa sasa


Friday, March 3, 2023

MATOKEO YA TOP TEN SHOW MSHINDI WA 8 NA WA 7...Varda Arts na Super Matimila

 Katika mtiririko wa washindi wa Top Ten Show, Mwenyekiti wa jopo la majaji Dr Alex Khalid aliwatangaza Varda Arts na wimbo wao Tazama Tanzania kuwa ni washindi wa 8, na Super Matimila na wimbo wao Muziki asili yake wapi kuwa washindi wa 7. Sikiliza hapa live kilichojiri siku hiyo.......kumbukumbu kutoka maktaba ya John Kitime


Thursday, March 2, 2023

MATOKEO YA WASHINDI WA TOP TEN SHOW...SIKILIZA MSHINDI WA 10 NA WA 9

 MOJA ya changamoto ya TOP TEN SHOW  ilikuwa ni urefu wa mashindano yenyewe yalianza mwaka 1988 na kuisha mwishoni mwa mwaka 1989. Sikiliza hapa jinsi walivyotajwa washindi na nyimbo walizopiga live baada ya kutajwa.

10. Orchestra Safari Sound Ndekule - Elimu ni msingi wa maisha

9. Mwenge Jazz band - UKIMWI

Toa maoni ............



Wednesday, March 1, 2023

HOTUBA YA DR ALEX KHALID KWENYE FAINALI YA TOP TEN SHOW 1988, UTADHANI ANAONGELEA HALI YA LEO (Part 1)

MWISHONI  mwa mwaka 1989 na mwanzoni mwa 1990 lilifanyika shindano kubwa la kupata nyimbo bora lililojulikana kama Top Ten Show. Bendi nchi nzima zilishiriki, RTD ilipita mikoa mbalimbali na kurekodi maonyesho 'live' ya bendi ambazo zilikuwa ndani ya mashindano hayo. Hatimae siku ya kilele ilifika, sasa hebu sikiliza hapa uchambuzi wa mwenyekiti wa jopo la majaji wa shindano lile Marehemu Balozi Dr Alex Khalid akichambua yaliyojiri, utadhani anaongelea muziki wa dansi leo, miaka 42 baadae. 

Je ina maana bendi bado ziko palepale zilipokuwa 1988?

 Toa maoni yako



Tuesday, January 10, 2023

MAQUIS ORIGINAL WAJIKUSANYA TAYARI KWA MAONYESHO MAKUBWA MAWILI YA PAMOJA

MAMBO MATAMU YAJA
BENDI kongwe iliyokuwa maarufu sana, Maquis Original itauanza mwaka huu kwa kufanya maonyesho mawili makubwa ya kumbukizi ya enzi zake. Maquis Original awali ilikuwa ikiitwa Maquis du Zaire wakati ikiingia nchini Tanzania kwa mara ya kwanza, ilikuwa ikitokea  mashariki ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, wakati huo nchi hiyo ikiitwa Zaire.
 Baada ya kuwasili Tanzania, haikupita muda mrefu bendi ikawa moja ya bendi tishio nchini. Nyimbo za bendi hii hata zile ilizo rekodi mwanzoni baada ya kuingia nchini bado ni nyimbo pendwa kwa waliokuweko enzi hizo na hata ambao wamezaliwa miaka mingi baada ya bendi kuwa imepotea katika ulimwengu wa muziki. Uamuzi wa wanamuziki wa bendi hii kujikusanya na kufanya maonyesho yao hakika ni faraja kubwa kwa wapenzi wa bendi hii. Bendi itafanya maonyesho mawili. Onyesho la kwanza litakuwa tarehe 21 Januari 2023 katika ukumbi wa Break Point Makumbusho na tarehe 27 January katika ukumbi wa Royal Village Dodoma

Hebu tukumbuke enzi hizo kwa kuangalia tangazo la dansi la Orchestra Maquis miaka hiyo ambalo nina uhakika litaleta kumbukumbu kwa wapenzi wa Maquis wa enzi hizo za Mtindo wa Telemka Chekecha Scania LBT III, wakati huo gari za Scania ndizo zilikuwa maarufu nchini na Scania LBT III ilikuwa gari yenye saiz kubwa kuliko zote, na ndio yenye kusifika zaidi. Maquis walikuwa na ufadhili wa kampuni hiyo ya magari, ukumbi wa nyumbani wa bendi hii wakati huo ulikuwa ukumbi wa White House uliokuwa Ubungo. Karibuni tena wapenzi wa White House mchangie, mambo yalikuwa mazito chini ya uongozi wa Chinyama Chiyaza ambae alikuwa mpiga Saxophone katika bendi. Wakati huu Maquis ilikuwa na maendeleo makubwa sana ya kuwa na mashamba, magari, matrekta na hata kuwa na Kota zake pale Sinza Palestina. Hebu angalia majina ya wanamuziki waliokuwa kwenye bendi hiyo, wote walikuwa miamba ya muziki.

MWAKA MPYA NGUVU MPYA


 

Thursday, December 22, 2022

WASIFU WA MAREHEMU RAMADHANI KINGUTI - KINGUTI SYSTEM

 


Marehemu Ramadhan Maulid Kinguti maarufu kama Kinguti System ni mzaliwa Ujiji, Kigoma. Alikuwa mtu aliyependa sana utani na ucheshi.

Bendi yake ya kwanza aliyojiunga mwaka 1977, ilikuwa Super Kibisa iliyokuwa na makao yake makuu Kigoma. Super Kibisa  ni bendi iliyoanzishwa mwaka 1968 pale Kigoma. Mwaka 1977 kiongozi wa bendi alikuwa Mlolwa Mussa Mahango ambaye alikuwa ni binamu yake Ramadhani Kinguti, na  hivyo ikawa rahisi  kwake kujiunga na bendi ile. Super Kibisa ilikuwa mali ya watu watatu, Gollo Saidi, Haruna Mahepe, na Maulidi. Katika bendi ya Super Kibisa, kipaji cha utunzi cha Kinguti kilianza  kujitokeza mapema na aliweza kutunga nyimbo kadhaa kama vile Kazi ni uhai, Mapenzi tabu,na Zaina.

Miaka miwili baadae, 1979, Kinguti alichukuliwa na Ahmed Sululu ambae alikua Katibu wa bendi ya  Dodoma International na kuhamia Dodoma. Dodoma International ilimchukua Kinguti ili kujaza nafasi ya Shaaban Dede ambaye alikuwa kahama bendi hiyo na kuhamia JUWATA.

Alipofika Dodoma international , Kinguti  alikutana kwa mara ya kwanza na mpiga gitaa mahiri marehemu Kassim Rashid. Kinguti aliiacha Dodoma International Orchestra na kujiunga na  Orchestra Makassy ambapo wakati huo walikuweko wanamuziki akina Marehemu Masiya Radi, mwimbaji  Mkongo ambaye alifariki kwa kukanyagwa na daladala maeneo ya Kinondoni Mbuyuni. Baadhi ya wanamuziki wengine ambao Kinguti alikuwa nao alipokuwa Orchestra Makassy walikuwa marehemu  Remmy Ongala, marehemu Andy Swebe, Keppy Kiombile, John Kitime, marehemu Issa Nundu, marehemu Kyanga Songa, Choyo Godjero na wengineo, pia alikuweko marehemu Aimala Mbutu kwenye solo, na Kassim Mganga (babake wa mwanamuziki wa Bongo flava Kassim Mganga-Milionea wa Mahaba) kwenye rhythm, na wengine wengi.  Kwa kipindi fulani muda huu Kinguti akiwa na wenzake chini ya Mzee Makassy wakafanya ziara ndefu nchini Kenya, kati ya waliokuwepo katika safari hiyo ni Nico Makoli,  Keppy Kiombile, Andy Swebe, Mzee Aimala Mbutu, Mzee Liston na wengine wengi akiwemo Mzee makassy mwenyewe.

1986 alijiunga Afrisongoma chini ya Lovy Longomba, hapa alitunga nyimbo kadhaa kama Pesa ni maua, Amana mpenzi, Estah Usituchonganishe, waimbaji wakati huo walikuwa Kinguti, marehemu Lovy Longomba  na Anania Ngoliga, kwenye solo alikuweko marehemu Kassim Mponda, na rhythm Maneno Uvuruge. Kwa muda mfupi alikuwa DDC Mlimani Park, na hapa akatunga kile kibao maarufu Visa vya mwenye nyumba, ambapo aliimba na Hassan Bitchuka, Francis Lubua, Hussein Jumbe na Benno Villa. Mwaka 1989 alikuwa moja ya wanamuziki waanzilishi wa Bicco Stars Band akiwa na Mafumu Bilali, Asia Darwesh, Andy Swebe, Mzee Aimala Mbutu, walitikisa na vibao kama Muuza chips, Leyla, Magreth maggie, Kitambaa cha kichwa, Nyumba ya kifahari, na nyingine nyingi tu. 1999 alijiunga na kilimanjaro Connection, alikaa bendi hii iliyokuwa chini ya Kanku Kelly kwa miaka miwili kisha kuanzisha bendi akiwa na Hassan Shaw, bendi iliyoitwa The Jambo Survivors ambayo wengi hapa Tanzania wataikumbuka kwa kibao cha Maproso. Bendi ya Jambo Survivors ikiwa bado na Ramadhan Kinguti na Hassan Shaw, kwa miaka kadhaa ikahamia Thailand. Baada ya kurudi Thailand afya ya Kinguti ilikuwa na migogoro mingi hivyo hakurudi tena kwenye muziki na muda mwingi alikuwa Dar es Salaam kisha Kigoma.

Ramadhani Kinguti amefariki tarehe 21 Disemba 2022 katika hospitali ya Maweni Kigoma, na mazishi ni tarehe 22 Disemba 2022 hapohapo Kigoma

Mungu amlaze Pema.

Sunday, December 18, 2022

TWO DAYS AFTER REMMY ONGALA DIED, HIS DRUMMER FOLLOWED HIM

The late Abou Semhando.

It was around three o'clock at night, on Saturday 18 December 2010, when I got a call from veteran musician Luiza Nyoni, she was crying and told me that there had been an accident and Abou Semahando who was on a motorcycle had been hit by a car and had died, the accident had happened in Mbezi Tanki Bovu. I woke up and went to the accident site and alas the information was true. I found Abou's motorcycle had already been loaded in a police car and the car that had hit him was in the ditch.  

In the accident, a van hit him in the back while he was on his motorcycle on his way home after a performance by his band, somewhere in  Africana area. According to his fellow musicians, Abou last played the drums for the second last song and decided to go home, minutes later got into a fatal accident. The strange thing is that Abou on his motorcycle led the funeral procession of Dr. Remmy Ongala just two days before his death..

The car involved in the accident

Abou's mangaled
 motorcycle

The car 

Abou Semhando first on right with a red shirt, in a group photo with fellow musicians during the Dr Remmy's funeral ceremony

Timetable for funeral arrangements for the late Abou Semhando (Baba Diana), musician and manager of the African Stars Band-Twanga Pepeta

• Saturday 18/12/2010-friends and relatives gathered at the home of the deceased, Mwananyamala Kisiwani (Ngilangwa) to offer condolences and console the bereaved.

• Sunday 19/12/2010- 5:00 AM.  Dawn prayers at  Muhimbili mosque, after the prayer the mourners would travel to Kibanda, Muheza ready for the funeral.

• Immediately after lunch the body would be moved to the Muheza mosque and after prayer the body would be taken to the cemetery for burial.

• Mourners would return to Dar es Salaam after the burial.

Some notable things:

1.19/12/2010 was  the day his eldest daughter was to be married

2. He had written to the management of the Band to give him a month's leave because he wanted not to be on stage for a while. It is the first time he wrote a letter requesting leave

3. The ringtone he put on his phone is the song by Njohole Jazz Band - this band's musicians almost all died together in a bad car accident.


Standing from left to right -.Remmy Ongala, Abuu Semhando,Kasaloo Kyanga, Fan Fan they are all deceased.

I first met Abou Semhando around 1979, we were both working with Printpak Tanzania Ltd, he was in typesetting department I was a proofreader. At the time he was with Sola TV Band I was with the Oshekas Band, but I would honestly say we were not close in any way. In 1989 I joined the Vijana Jazz band he was the band's second in command and we became quite close after. In his lifetime Abou was a member of several bands including Sola TV, Vijana Jazz, Diamond Sound and Super Matimila.
In the evening after DR Remmy's burial,
 Abou Semhando and Cosmas Chidumule, a veteran musician who was once also a member of Super Matimila Band under Dr Remmy Ongala,Semhando were joking about who would follow after the death of their colleague.

Abou Semhando : You will follow and back his songs like you always did.

Cosmas Chidumule: No way, you should follow him after all you were his drummer for a longer period.

Two days later it was a joke no more Abou went on to join his comrade

MAY GOD FORGIVE THEIR SHORTCOMINGS 

AMEN